Generation Xix

TXT

TOURISM

NMB

TTCL

TTCL

Friday 11 January 2013

Ndoto ya kufufua ATCL itimie, nchi iwe na shirika lake la ndege

KWA muda wa zaidi ya miaka 10 sasa kumekuwako na mjadala mkali juu ya hatima ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) hasa uwezekano wa kulifufua ili liweze kuendelea na shughuli zake kama kawaida.
Mbali na mjadala ndani ya jamii kuhusu mustakabali wa ATCL, pia viongozi serikalini kwa nyakati tofauti nao wamekuwa wakitoa ahadi za kufufua na kuimarisha ATCL iweze kutoa huduma zake ndani na nje ya nchi kama ilivyokuwa enzi za uongozi wa Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere.
Ni jambo la aibu na kusikitisha kwamba kama taifa lenye rasilimali zote ambazo nchi imebarikiwa kuwa nazo, tumeshindwa kabisa kufufua ATCL na hasa pale ahadi lukuki zinapotolewa bila ya kutimizwa.
Maoni yetu leo yanazidi kusisitiza kwamba ndoto ya kufufua ATCL itimie ili tuweze kuwa na Shirika la Ndege. Tunasema hivi kwa sababu sifa ya kuwa na Shirika la Ndege ni kuwa na ndege za kutosha na kutoa huduma hiyo ya usafiri wa anga bila matatizo. Tofauti na hivyo, tutaendelea kudanganyana kwamba kuna Shirika la Ndege nchini wakati hatuna.Ndiyo maana taarifa za kwamba umoja wa wafanyabiashara wa Oman wapo katika mchakato wa kukamilisha uwekezaji wa Sh160 bilioni kwa ATCL zinaongeza matumaini kuwa huenda nchi ikarejea kuwa na Shirika la Ndege.
nuhu85

No comments: