SHIRIKA la Ndege la Precision Air linatarajia kuzindua safari za kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya kuanzia Ijumaa ijayo.
Hatua hiyo inafuatia kukamilika kwa ujenzi wa Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Songwe mkoani Mbeya.
Hatua hiyo inafuatia kukamilika kwa ujenzi wa Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Songwe mkoani Mbeya.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika 
ofisi za makao makuu ya shirika hilo jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa 
Idara ya Masoko na Uhusiano, Linda Chiza alisema abiria wa safari hiyo, 
watahudumiwa na ndege aina ya ATR-72, yenye uwezo wa kubeba abiria 70.
Alisema kwa mujibu wa ratiba ya shirika, ndege 
hiyo itakuwa inaruka mara nne kwa wiki kwenda Mbeya na kwamba safari 
hizo zitaongezeka kwa kadri njia hiyo itakavyoimarika.
“Lengo ni kuwapa abiria wetu unafuu wa kuchagua muda wa kusafiri unaowafaa kulingana na ratiba zao,” alisema Linda.
“Tunajivunia kuzindua safari hii mpya kuelekea 
Mbeya ambayo itatuwezesha sasa kuwapatia huduma abiria kutoka Mbeya na 
Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.  Alielezea matumaini ya shirika lake kuwa
 kwa kupeleka huduma hizo mkoani Mbeya, litakuwa  linarahisisha usafiri 
kwa watalii, wafanyabiashara na  watu wengine wanaopenda kutembelea mkoa
 huo wenye utajiri wa vivutio vya utalii.
Vivutio hivyo ni pamoja na  Mbuga ya Taifa ya Wanyama ya Ruaha na Katavi na Hifadhi nyingine nyingi za taifa.
nuhu85
 
 
 

 
 



